Ad Code

TANGAZA NA KANKONO MEDIA HAPA 0659671919

BALOZI MSTAHAFU DR.SLAA MIKONONI MWA JESHI LA POLISI




BALOZI MSTAHAFU DR.SLAA MIKONONI MWA JESHI LA POLISI

kankonomediablogspot.com Januari 10.2024 - DAR ES SALAAM 



JESHI la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, linamshikilia kwa mahojiano aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweeden, Dk Willibrod Slaa.



Slaa alikamatwa usiku wa kuamkia leo Januari 10,2025 nyumbani kwake Bweni. Mpaka sasa Jeshi hilo halijaweka wazi tuhuma zinazomkabili mwanasiasa huyo ambaye pia aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Karatu.


Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro,amethibitisha kukamatwa kwa Dk. Slaa na kueleza kuwa mahojiano  yamekwenda vizuri na hivi sasa wanaangalia sheria zinasemaje ili wachukue  hatua zaidi.


Hata hivyo kamanda Muliro hakuwa tayari kueleza kwa undani tuhuma zinazomkabili.



#KankonoMediaNewsUPDATES

Post a Comment

0 Comments